Song Ndoto Ya Mchana Lyrics

Full Translation of Song Ndoto Ya Mchana Lyrics on e akhabaar.

Verse 1

Niliskia tufununu, Kwamba ulipata mwingine,

Anayekupenda zaidi ya mimi, mtafunga ndoa

pengine,

Yetu ilikuwa shadow, mapenzi yenu yamekolea,

Lazima huwa Anakupa, vitu sikuwa nakupea,

Ndoto zako zote, ulizoniambia,

Naona kama kweli sasa zinatimia,

Na Sina chochote, cha kukuambia,

Ila nakonda Kweli nikikufikiria,

Hook

Sura yako umbo lako jamani eeh,

Busu na mahaba chumbani maami ,

Mawaidha yako nikiwa matatani eeh,

Nikikumbuka najiona hayawani maami

Chorus:

Nawatakia mema, (Nawatakia mema)

Nawatakia mema, (Nawatakia mema)

Nawatakia mema, (Nawatakia mema)

Basi kwaheri kwaheri kwaheri Mami (Ndoto

yangu ya Mchana)

Ingawa inaniuma, niko na furaha moyoni,

Kuona kwamba umepata, vyote ulivyokuwa

unatamani,

Naomba nipate mwaliko, wa harusi nije Nile wali,

Nipige picha na wadau, nikupe zawadi kama

zamani

Alafu ntapeform, kama beshte yako, kale

kawimbo nilikuimbia shambani

Na nitakuinform, tunza mume wako, Japo kuna

vitu zenye ninatamani,

Hook:

Chorus

Ingawa ningependa,ungekuwa wangu pekee,

(Nawatakia mema)

Ingawa moyoni umeniachia kidonda, (Nawatakia

mema)

Namwomba Mungu, anipatie mwingine Kama

wewe, (Nawatakia mema)

Hivo kwaheri kwaheri kwaheri kwaheri mama

(Ndoto yangu ya Mchana)

Lakini ninaomba, unifanyie favour Moja

(Nawatakia mema)

Ukijifungua kama ni wa kiume,mpe jina laangu

(Nawatakia mema)

Na kama ni wa kike mpe jina la mama yangu

(Nawatakia mema)

Basi kwaheriiiiiiii (Ndoto yangu ya Mchana)

Write Your favorite line from Song Ndoto Ya Mchana Lyrics below in the comments